Job 42:1-6

(Ayubu 42)

Ayubu Anamjibu Bwana

1Ndipo Ayubu akamjibu Bwana:
2 a“Ninajua ya kuwa unaweza kufanya mambo yote,
wala hakuna mpango wako unaoweza kuzuilika.

3 bUliuliza, ‘Ni nani huyu afichaye mashauri yangu bila maarifa?’
Hakika nilisema juu ya mambo niliyokuwa siyaelewi,
mambo ya ajabu mno kwangu mimi kuyajua.


4 c“Ulisema, ‘Sikiliza sasa, nami nitanena;
nitakuuliza swali, nawe yakupasa kunijibu.’

5 dMasikio yangu yalikuwa yamesikia habari zako,
lakini sasa macho yangu yamekuona.

6 eKwa hiyo najidharau mwenyewe,
na kutubu katika mavumbi na majivu.”

Mwisho: Marafiki Wa Ayubu Wanafedheheshwa

Copyright information for SwhKC