Job 42:1-6
(Ayubu 42)
Ayubu Anamjibu Bwana
1Ndipo Ayubu akamjibu Bwana:2 a“Ninajua ya kuwa unaweza kufanya mambo yote,
wala hakuna mpango wako unaoweza kuzuilika.
3 bUliuliza, ‘Ni nani huyu afichaye mashauri yangu bila maarifa?’
Hakika nilisema juu ya mambo niliyokuwa siyaelewi,
mambo ya ajabu mno kwangu mimi kuyajua.
4 c“Ulisema, ‘Sikiliza sasa, nami nitanena;
nitakuuliza swali, nawe yakupasa kunijibu.’
5 dMasikio yangu yalikuwa yamesikia habari zako,
lakini sasa macho yangu yamekuona.
6 eKwa hiyo najidharau mwenyewe,
na kutubu katika mavumbi na majivu.”
Mwisho: Marafiki Wa Ayubu Wanafedheheshwa
Copyright information for
SwhKC